• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Thursday, 6 July 2017

    Zambia yaendeleza ubabe kwa Taifa Stars Cosafa Cup 2017.

    Cosafa Cup imeendelea Julai 5, 2017 ambapo Taifa Stars ya Tanzania imekutana na timu ya Taifa ya Zambia kwenye hatua ya nusu fainali ya mashindano ya mwaka huu.
    Taifa Stars imeshindwa kusonga mbele kwenye mashindano ya Cosafa baada ya kupoteza mchezo kwa kufungwa 4-2 na kuiacha Zambia ikisonga mbele kucheza fainali ya michuano hiyo nchini Afrika Kusini.
    Magoli ya Stars yamefungwa na Erasto Nyoni dakika ya 14 ambaye alifunga goli la kwanza kisha Simon Msuva akafunga goli la pili dakika ya 85 wakati magoli ya Zambia yakifungwa na Mwila dakika ya 44 kisha Shonga akafunga dakika ya 45+2 Zambia wakapata goli la tatu kwa mkwaju wa penati uliofungwa na Chirwa dakika ya 56 halafu Shonga akafunga bao la nne likiwa ni goli lake la pili dakika ya 68.



    No comments:

    Post a Comment