• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Thursday, 6 July 2017

    Tanzania na nyota njema ya kupanda viwango vya Fifa.

    Taarifa iliyotolewa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani Leo Julai 6, 2017 inahusu kupanda na kushuka kwa viwango vya soka kwa timu za mataifa mbalimbali,huku Tanzania ikipanda katika viwango vya soka kwa mwezi June baada ya kufanya vizuri katika michezo kadhaa.
    Tanzania imepanda kutoka nafasi ya 139 hadi nafasi ya 114, ikiwa imepanda kwa nafasi 25. Hiyo ni inakuja kama chachu na taarifa nzuri kwa soka la Tanzania ambapo inatoa nafasi kwa kuonesha mataifa mengine kuwa soka la Tanzania linakua kwa kasi.


    Ingawaje changamoto hazikosekani lakini angalau sasa Tanzania imaendelea kuweka vielelezo madhubuti katika kuinuka kisoka kadiri siku zinavyokwenda.

    No comments:

    Post a Comment