• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Monday, 19 June 2017

    Waziri Mwigulu Nchemba amewaomba Watanzania kuweka Imani na Kumuombea Kwa JPM.

    Waziri Mwigulu Nchemba amewataka Watanzania kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli katika kuendelea kulinda rasilimali tulizonazo nchini, ameyasema hayo alipokuwa kwenye ziara Jimboni kwake Iramba Magharibi amewaomba Watanzania kuungana katika kumuombea Rais,na viongozi wote wenye nia njema na moyo wa uzalendo ili juhudi za kulinda na kusimamia rasilimali za Taifa zinazoongozwa na Rais JPM zipate mafanikio na baraka za watanzania wote.

    Kwa mtanzania yeyote mwenye mapenzi mema na nchi yetu lazima ataunga mkono juhudi hizo lakini kwa ambaye ana mambo yake ya ubinafsi na ametanguliza ubinafsi anaweza asielewe kazi inayofanywa lakini sisi ambao tunahitaji maji; tunaohitaji barabara, tunaohitaji elimu bure, tunaohitaji Hospitalini dawa ziwepo, tunaohitaji umeme, sote kwa maombi na kwa jitihada na hata kwa kusema tumuunge mkono Rais wetu kwa uzalendo na ujasiri mkubwa aliouonesha”.

    Kwa imani zetu wote, tuendelee kumuombea Rais wa nchi yetu, Rais wetu mpendwa kwa kazi kubwa anazozifanya ambazo zitasaidi hii mipango mingi tunayopanga kwenye majimbo yetu, matamanio na matarajio yetu mengi tunayokuwa nayo katika majimbo yetu”.alisisitiza Mwigulu Nchemba.



    No comments:

    Post a Comment