• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Monday, 19 June 2017

    Ureno vs Mexico hakuna mbabe,Cameroon yachezea kipigo toka kwa Chile.

    Ni burudani isiyo na kifani imeendelea kuonekana kwenye michuano ya kombe la mabara ambapo siku ya pili ya michuano hiyo inayoendelea huko nchini Urusi.

    Katika kundi A timu ya taifa ya Ureno walitoshana nguvu na Mexico kwa sare ya mabao 2-2, Ricardo Quaresma alianza kuipatia Ureno goli la kuongoza katika dakika ya 35
    Mexico walisawazisha goli hilo kupita kwa “Javier Hernandez” Chicharito na kumfanya mshambuliaji huyu kuwa ndio mfungaji bora wa muda wote wa timu ya taifa akifikisha mabao 48.
    Beki Cedric Soares akaongeza bao la pili kwa Ureno katika dakika ya 86 kabla ya Hector Moreno kusawazisha goli hilo kwa upande wa Mexico katika dakika za lala salama.
    Katika mchezo wa kundi B wawakilishi wa bara la Afrika Cameroon walichapwa na mabingwa wa Amerika ya kusini, Chile kwa mabao 2-0 mabao ya Chile yalifungwa katika kipindi cha pili na Arturo Vidal na Eduardo Vargas.

    No comments:

    Post a Comment