• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Monday, 26 June 2017

    Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa atoa onyo usafirishaji wa chakula kwenda nje ya Nchi.

    Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa amepiga marufuku usafirishaji wa chakula kwenda nje ya nchi.

    Waziri mkuu Majaliwa amesema yeyote atakayekamatwa akijaribu kusafirisha chakula nje ya nchi hiyo, chakula hicho kitataifishwa na kupelekwa ghala la taifa.amesema hayo wakati akitoa nasaha kwenye Baraza la Eid lililofanyika kitaifa kwenye msikiti wa Masjid Riadha, mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro mara baada ya kuswali sala ya Eid, waziri mkuu huyo alisema serikali imechukua hatua hiyo kuzuia Tanzania isikumbwe na baa la njaa.

    "Kuanzia leo, ni marufuku kwa mtu yoyote kusafirisha mazao ya chakula kwenda nje ya nchi bila ya vibali. Serikali inahamasisha uwekezaji kwenye ujenzi wa viwanda nchini. Kama tutatoa vibali, ni lazima mtu alazimike kusaga nafaka ili kutoa ajira nchini,” akaongeza kwa kusema " Mimi nasema kuanzia leo, yeyote atakayekamatwa akitorosha chakula kwenda nje ya nchi, chakula hicho kitataifishwa na kupelekwa ghala la Taifa na gari lake tutalitaifisha na litaishia Jeshi la Polisi. Tunafanya hayo kwa lengo la kuwalinda Watanzania tusikumbwe na baa la njaa”.


    Ametanabaisha kuwa mipaka ya Tarakea, Holili, Mwanga, Horohoro, Siha, Namanga na Sirari imekuwa inapitisha kiasi kikubwa cha mazao ya chakula kwenda nje ya nchi jambo ambalo ni hatari sana. Lakini pia waziri mkuu huyo amewataka wafanyabiashara wa ndani ya nchi ya Tanzania, wachukue mahindi kutoka maeneo yenye mavuno mengi na kuyapeleka kwenye sehemu zenye mavuno kidogo.

    No comments:

    Post a Comment