• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Monday, 26 June 2017

    Mwigulu Nchemba-Wanaotaka haki za ushoga na Ruksa ya Mimba mashuleni watafute Nchi yao,sio Tanzania.

    Waziri wa mambo ya ndani wa Tanzania Mwigulu Nchemba amesema kama kuna taasisi yoyote imesajiliwa nchini na inafanya kampeni za haki za ushoga basi atafuta usajili huo na watu wake kukamata na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

    "Wanaotaka haki za ushoga watafute tu nchi yao nyingine ambayo inaruhusu mambo hayo wakakae huko, kama ni taasisi imesajiliwa kwenye nchi yetu tukaigundua inafanya kampeni ya haki hizo na bahati nzuri zinasajiliwa Wizara ya Mambo ya Ndani nitazifutia usajili wao”.

    "kama ni raia wa Tanzania anaendesha kampeni hizo tutamkamata na kumfikisha kwenye vyombo vya sheria, na kama si raia amekuja kwenye nchi yetu kuja kuendesha haki hizo tutampa amri ya kuondoka ndani ya nchi yetu hatapata fursa hata ya kuchomoa chaji ya simu kwenye soketi ya umeme”.


    Pia Waziri Nchemba ameunga mkono kauli,na maelekezo ya Rais Magufuli dhidi ya wanafunzi ambao watapata ujauzito wakiwa shuleni na kusema watu wanaopinga jambo hilo wasitumie nguvu kubwa kupinga bali wajenge shule zao watoe hiyo haki ya kusomesha wanafunzi wajawazito au wale ambao tayari wamejifungua na siyo kulazimisha serikali kufanya hayo.

    No comments:

    Post a Comment