• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Friday, 16 June 2017

    Vanessa Mdee ndani ya XXL ya Clouds FM,amefunguka kwa kusema maisha yanagusa sanaa na sanaa inagusa maisha.

    Msanii na mwimbaji wa Bongofleva Vanessa Mdee”V Money” akiwa kwenye kipindi cha XXL ya Clouds FM leo juni 16 2017 amesema kuonekana kwake kwenye video akiwa anawabusu mwanaume ni sehemu ya kazi tu na si vinginevyo.

    Vanessa ameyasema hayo wakati anaelezea namna alivyoonekana kwenye Red Carpet ya tuzo za Billboard na jinsi alivyopata deal la kuigiza Tamthiliya ya Shuga na kuelezea namna alivyoonekana akikiss na mwanaume mwingine kwenye Tamthiliya hiyo.

    Jamani ile ni kazi,Halafu mimi ni muigizaji na Kwenye Shuga nimeigiza na hiyo show ina mafunzo kama mtu akiangalia kwa makini atajifunza kitu kikubwa sana.Nawasihi wadogo zangu na Watanzania wakaiangalie watapata kitu.


    Hata Jux anajua kuwa ile ni kazi,kwani hata nae ,huwa inatokea akiwa na mademu wake huko kwenye ma-video wanashikana shikana,kwahiyo sio kama nalipiza la hasha, sema kila kitu kwenye maisha kimegusa sanaa na sanaa imegusa maisha.”aliongeza Vanessa.

    No comments:

    Post a Comment