• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Saturday, 17 June 2017

    Timu za michuano ya mabara” Confedaration Cup” zinaanza kusugua daluga leo.

    Michuano ya mabara"Confedaration Cup” inayoanza siku ya leo june17 nchini Russia,ambapo wenyeji Russia watachuana na New Zealand kwenye mchezo wa ufunguzi wa mashindano hayo.
    Mchezo huu kati ya Russia na NewZealand unatarajiwa kupigwa kwenye uwanja wa St Petersburg uwanja wa nyumbani wa klabu ya St Petersburg.

    Timu ya taifa ya Ureno wataliwakilisha bara la Ulaya kama mabingwa wa bara hilo huku waandishi wa habari wakiwa wamepiga kambi katika timu hiyo kufuatilia mkasa mkubwa wa kodi unaomuandama Cristiano Ronaldo.

    "Ronaldo ameonekana kuichukulia umuhimu michuano hii na hawazi yanayotokea nje ya uwanja kwani akili yake yote iko katika michuano hii tu"


    Inasemekana tangu ishu ya Cristiano Ronaldo kusemekana anakwepa kodi kutawala vyombo vya habari ,Jamaa ameonekana kukosa raha na huenda anafikiria kuondoka nchini Hispania kwenye klabu yake ya Real Madrid,june18 ureno watashuka dimbani dhidi ya Mexico.

    No comments:

    Post a Comment