• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Saturday, 17 June 2017

    Prof. Anna Tibaijuka Ameomba serikali kuwapunguzia wakazi wa bukoba gharama za vifaa vya ujenzi.

    Mbunge wa Muleba Kusini Prof. Anna Tibaijuka alisimama Bungeni mjini Dodoma mwishoni mwa wiki kuchangia kwenye Bajeti Kuu ya Serikali inayoendelea kujadiliwa kwa mwaka wa fedha 2017/18.

    Aidha ameomba serikali iwaangalie watu wa kagera kwa jicho la tatu hasa kwenye bidhaa zote zinahusika kwenye vifaa vya ujenzi,ili watu wa kagera waweze kujenga na kufanya marekebisho ya nyumba zao zilizoharibiwa na tetemeko la ardhi.

    Ameshukuru pia kwa kuondolewa kwa kodi kadhaa kwenye mazao,pia mabenki yamewezeshwa lakini pia tuangalie zaidi kwa upande wa bima ili ziwe msaaada mkubwa zaidi kwa watu wetu.


    Ameomba pia serikali iendelee kutoa ruzuku mbalimbali kwenye maeneo tofauti hasa kwenye eneo la kilimo,amesema bajeti ni nzuri na imelenga kuwasaidia watu wa chini kwa kiwango cha juu,hivyo huenda ikaleta tija kwa maendeleo ya taifa.

    No comments:

    Post a Comment