• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Saturday, 17 June 2017

    Tanzania yatajwa kwenye listi ya nchi zinazokua kiuchumi kwa kasi duniani.

    Tanzania imeendelea kuonekana ni moja ya nchi zinazoendelea kukua kiuchumi kwa kasi ,na kwa kupitia ripoti iliyotolewa na Benki ya Dunia (WB) na imewekwa list ya nchi ambazo zinakuwa haraka kiuchumi mwaka 2017 hasa kwa kuonekana kuimarisha biashara na miundombinu.
    Katika list hii Ethiopia inakamata nafasi ya kwanza ambapo uchumi wake umekua kwa 8.3% huku Tanzania ikitajwa miongoni mwa nchi 10 ikikamata nafasi ya 5 uchumi wake ukikua kwa 7.2% huku uchumi wa Djibouti ukikua kwa 7% licha ya kukabiliwa na ukame mkubwa.

    "Baaada ya kuwepo kwa taarifa iliyoionesha Tanzania kuwa miongoni mwa nchi ambazo uchumi wake unaendelea kukua kwa kasi duniani,wadau mbali mbali wameeleza huenda usimamizi mzuri wa rasilimali kwenye awamu ya tano ya uongozi wa nchi hiyo huenda ndio ukawa ni chachu ya kuinuka kwa uchumi".

    "huku ikitajwa kuwa harakati za kuzuia na kupambana na vitendo vya rushwa na ufisadi vimezidi kuimarisha utendaji kazi na msukumo wa kizalendo miongoni mwa watumishi na raia wa taifa hilo,lililopo Afrika ya mashariki".





    No comments:

    Post a Comment