• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Sunday, 18 June 2017

    Stim tosha vs Makuburi SC hakuna mbabe ufunguzi wa Ndondo Cup 2017.

    Mchezo wa ufunguzi ya hatua ya makundi michuano ya Ndondo Cup 2017 Makuburi SC vs Stim Tosha imemalizika kwa sare na kupelekea timu hizo kugawana pointi,mchezo ulikuwa ni wa hali ya juu huku kila timu ikiliandama goli la mwenzake ili kuzitafuta pointi tatu.

    Shangwe kubwa toka kwa Mashabiki waliojitokeza kwenye uwanja wa Kinesi kwa ajili ya kushuhudia pambano hilo ambapo kulikua na burudani kibao kutoka kwa wasanii wa muziki wa Kisingeli (Sholo Mwamba, Man Fongo pamoja na Moto Kombati “mwendo wa mateka”


    Mashabiki waliweza kuonesha ustaarabu na nidhamu nzuri wakati wa mchezo na hata baada ya mchezo na imepelekea kuonesha utofauti mkubwa ,kwani wengi wamekua wakiamini Ndondo ni sehemu ya fujo na vurugu.lakini ndondo imeendelea kudhihirika kuwa ni sehemu ya burudani kwa wapenda michezo na burudani.

    No comments:

    Post a Comment