• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Sunday, 18 June 2017

    Moto wa nyika waleta maafa makubwa huko nchini Ureno.

    Nchini Ureno kumezuka moto mkubwa wa msituni katika maeneo ya katikati mwa nchi hiyo, na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 25 na kuwajeruhi wengine 20, wakiwemo maafisa kadhaa wa zima moto.
    Awali watu waliofariki walikuwa 19, lakini sasa idadi hiyo imepanda na kufikia 25. Wengi wao walifariki pale walipokuwa wakiukimbia mji wa Pedrogao Grande,na kuendelea kuvuta hewa yenye moshi mkali umbali wa kilomita 50 Kusini mashariki mwa Coimbra, wakitumia magari yao.
    Waziri wa maswala ya ndani wa nchi hiyo João Gomes, amewaambia waandishi habari kuwa, waathiriwa 16 wameteketea ndani ya magari yao hadi kufa, pale walipokabiliwa na moto huo mkubwa katika Wilaya ya Pedrógão Grande barabara inayounganisha miji ya Figueiro dos Vinhos na Castanheira de Pera.


    Haijabainika kilichosababisha moto huo wa msituni, ambao umeteketeza nyumba nyingi katika maeneo hayo na tayari baadhi ya nchi zilizoguswa na kutokea kwa janga hilo zimeanza kutoa msaada kwa kushirikiana ili kukabiliana na moto huo huku nchi kama Hispania ilituma ndege za kusaidia kuzima moto huo.

    No comments:

    Post a Comment