• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Monday, 19 June 2017

    Timu ya Taifa ya Ujerumani imeanza vyema,michuano ya Mabara Confederation Cup.

    Timu ya taifa ya Ujerumani leo walikuwa uwanjani katika mchezo wao wa kwanza wa michuano ya Confedaration Cup dhidi ya timu ya taifa ya Australia.
    Mchezo huo ulionekana kuwa na upekee ambapo Ujerumani walitangulia kupata bao la kwanza dakika ya 5 kupitia kwa Larsi Standi kabla ya Tom Rogic kuisawazishia Australia dakika ya 41 na dakika ya 45 Julian Draxler aliipatia Ujerumani bao la pili.

    Kipindi cha kwanza kiliisha kwa Ujerumani kuongoza bao 2 kwa 1 na katika kipindi cha pili dakika ya 48 Leon Goreztka aliiandika Ujerumani bao la 3 kabla ya Tomi Juric kuipatia Australia bao la pili.

    Matokeo hayo yanaifanya Ujerumani kuwa na pointi sawa na Chile ambao jana waliifunga Cameroon huku Australia na Cameroon wenyewe wakikosa pointi muhimu mpaka sasa.




    No comments:

    Post a Comment