• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Thursday, 22 June 2017

    Taifa Stars imesafiri kwenda kwenye mwaliko wa kushiriki michuano ya COSAFA.

    Taifa Stars imealikwa kwenye michuano iliyoandaliwa na Baraza la Mpira wa Miguu la nchi za Kusini mwa Afrika,ambapo Tanzania sio mwanachama wa Cosafa, lakini imepata mwaliko katika mashindano hayo yanayotarajiwa kuanza Juni 25, mwaka huu.
     Timu za Botswana, Zambia na Afrika Kusini kadhalika Namibia, Lesotho na Swaziland zitakuwa na mechi maalumu (play off) ili kuingia robo fainali,wakati Stars imepangwa kundi A ikiwa kundi moja na timu za Mauritius, Malawi na Angola ,majirani zetu Msumbiji wakiwa kundi B,pamoja na Shelisheli, Madagascar na Zimbabwe.
    Kwa mujibu wa Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Salum Mayanga, kikosi kinachoondoka leo ni makipa Aishi Salum Manula (Azam FC), Benno David Kakolanya (Young Africans SC) na Said Mohammed Said (Mtibwa Sugar FC).

    Safu ya ulinzi wapo: Shomari Salum Kapombe (Azam FC) na Hassan Hamis Ramadhan ‘Kessy’ (Young Africans SC) wakati upande wa kushoto wapo Gadiel Michael (Azam FC) na Amim Abdulkarim (Toto Africans FC), Erasto Nyoni (Azam FC), Salim Hassan Abdallah (Mtibwa Sugar), Abdi Banda (Simba SC) na Nurdin Chona (Tanzania Prisons) wakati viungo wa kuzuia kuwa ni Himid Mao (Azam FC) na Salmin Hoza wa Mbao FC.
    Upande wa viungo wapo: Mzamiru Yassin Selembe (Simba), Simon Happygod Msuva (Young Africans SC), Raphael Daudi (Mbeya City) na Shizza Ramadhani Kichuya (Simba SC).


    Nayo safu ya ushambuliaji wapo: Thomas Ulimwengu (AFC Eskilstuna – Sweden), Mbaraka Abeid Yusufu (Kagera Sugar), Stamili Mbonde, Elius Maguli (Dhofar SC) na Shabani Idd Chilunda (Azam FC).

    No comments:

    Post a Comment