• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Friday, 23 June 2017

    Lionel Messi na baba yake kuikwepa Jela kwa fungu la vitita vya faini.

    Mshambuliaji wa klabu ya Barcelona Lionel Messi na baba yake,wamenusurika kwenda jela baada ya kupatikana na hatia katika kesi iliyokuwa ikiwakabili ya ukwepaji kulipa kodi,na kutakiwa kulipa faini ikiwa ni mbadala wa vifungo vyao.
    Mwezi Julai mwaka jana Lioneil Messi na baba yake walikutwa na hatia katika kesi hiyo iliyokuwa ikiwakabili na baada ya hukumu waliamriwa kulipa faini au kutumikia kifungo.Messi na baba yake walihukumiwa kifungo cha miezi 21.
    Messi na baba yake waliajiri kundi la mawakili ambao walijaribu kuwatete katika kesi hiyo bila mafanikio na baadae mamlaka za kisheria zikawahukumu.Sasa taarifa zinasema Lioneil Messi amekubali kulipa faini ya euro 252,000 na baba yake akilipa euro 180,000 na hiyo itawafanya kuepuka kifungo kilichokuwa kinawakabili.


    Masta kadhaa wa soka wamekuwa wakikumbwa na tuhuma za ukwepaji kodi nchini Hispania ambapo Cristiano Ronaldo na kocha Jose Mourinho nao wapo katika uchunguzi.

    No comments:

    Post a Comment