• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Friday, 23 June 2017

    Polisi Dsm imewahakikishia wananchi amani na utulivu wa kutosha,kuelekea Sikukuu ya Eid.

    Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya DSM katika kuhakikisha linadumisha amani na hali ya usalama na utulivu kwenye msimu huu wa Sikukuu limesema litatumia vikosi vyake vyote kusimamia amani na usalama maeneo mbalimbali zikiwemo kumbi na sehemu zenye mkusanyiko wa watu wengi.

    Akizungumza na Waandishi wa Habari, Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum DSM Lucas Mkondya amesema Jeshi hilo limejipanga kuhakikisha Watanzania wanasherehekea vizuri Sikukuu.

    "Napenda kuwaambia kwamba Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya DSM tumejipanga vyema sana. Kwa hiyo Wananchi wajiandae tu kwa sherehe,Nyumba zote za Ibada tutaweka Askari. Kutakuwa na Askari wa kawaida wenye Uniform lakini pia kutakuwepo na Askari kanzu kufuatilia nani anataka kufanya vurugu katika nyumba za Ibada lakini pia katika sehemu ambazo Wananchi wataenda kufanya Sherehe".

    "Tunawaomba wananchi wawachunge watoto wao,madereva wasinywe pombe na wasingatie sheria za usalama barabarani pindi waendeshapo vyombo vyao vya moto,na wanaopendelea kwenda beach wawe makini na watoto,lakini pia wamiliki wa kumbi za starehe ni marufuku kuweka disko toto na watakaokiuka maelekezo watachukuliwa hatua kali mara moja".

    "Tutatumia katika kuhakikisha ulinzi unaimarika tutatumia Vikosi vyetu vyote. Tutatumia Vikosi vya FFU vitakuwepo mitaani kwa ajili ya kuimarisha Doria. Tutatumia Helkopta, tutatumia Farasi, tutatumia Mbwa na Askari wengi sana watakuwepo. Kwa hiyo napenda kuwahakikishia Wananchi kwamba wasiwe na wasiwasi Jeshi lao la Polisi limejipanga katika kuwalinda na kuhakikisha kwamba Sikukuu Eid Mosi, Eid Pili zinapita salama bila kubughudhiwa." aliongea kaimu kamanda wa kanda maalumu Dsm -Lucas Mkondya.




    No comments:

    Post a Comment