• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Friday, 23 June 2017

    Makuburi SC wawachakaza “Temeke market” mabingwa watetezi Ndondo Cup.

    Mabingwa watetezi wa kombe la Ndondo Cup Temeke Market wamechezea kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Makuburi SC kwenye mchezo wa Kundi G uliopigwa kwenye uwanja wa Kinesi pale maeneo ya Sinza Dar es Salaam.
    Mwinyi Ally alianza kuifungia bao Makuburi dakika ya 56 kipindi cha pili baada ya timu hizo kumaliza kipndi cha kwanza bila kufungana, Paul Ndauka akaisawazishia Temeke Market dakika ya 70 lakini wakati zimesalia dakika nane tu mechi imalizike Victor Hangaya akaifungia Makuburi bao la ushindi.
    Katika uwanja wa Mwl. Nyerere, Magomeni, Dar Police Collage wamepoteza mechi yao ya pili mfululizo kwenye Kundi G baada ya kufungwa 1-0 na Stim Tosha timu kutoka maeneo ya Mabibo. Dar Police Collage wamejiweka kwenye wakati mgumu wa kusonga mbele kwenye michuano hiyo wakiwa hawana hata pointi hadi sasa baada ya kucheza mechi mbili. 

    No comments:

    Post a Comment