• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Tuesday, 20 June 2017

    Shabiki namba moja wa mabingwa wa soka Tanzania bara Yanga afariki dunia.

    Mabingwa wa soka Tanzania bara kwa mara tatu mfululizo klabu ya Yanga wamepatwa na msiba mzito baada ya moja ya aliyekuwa mshabiki wao nambari moja kufariki.

    Shabiki huyo aliyekuwa akitambulika kama Ally Yanga amefariki hii leo mchana jijini Dodoma ambako taarifa zinasema alikuwa kwenye shughuli za kukimbiza mwenge,Ally Yanga alipata umaarufu sana kwa ushangiliaji wake wa kipekee kwa kujipaka “masinzi” ya mkaa usoni na kujaza nguo katika tumbo lake kama ana kitambi.

    Kutokana na msiba huo aliyekuwa msemaji wa klabu ya Simba bwana Haji Manara ametuma salamu za pole kwa watani wake hao na akisema amehuzunishwa na msiba huo. “nimepigiwa simu kwamba Ally Yanga amefariki huko Mpwapwa mkoani Dodoma,msiba huu ni wetu wote na tunawapa pole watani zetu.” aliandika Manara kwenye instagram akaunti yake.

    No comments:

    Post a Comment