• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Tuesday, 20 June 2017

    Nchi ya Tanzania imeonekana kubeba wakimbizi wengi toka Burundi.

    Tanzania ni nchi inayohifadhi wakimbizi wengi zaidi kutoka Burundi kuliko nchi nyingine katika ukanda wa Afrika Mashariki,Ripoti ya shirika la wakimbi la Umoja wa Mataifa UNHCR inasema hadi hivi sasa, kuna wakimbizi Laki 2 na 41 elfu waliopo kwenye kambi za wakimbizi nchini Tanzania wanatokea Burundi.
    Ripoti iliyoainisha kati ya kipindi cha miezi mitano,ya mwaka huu 2017, wakimbizi 44,487 wamekimbilia Tanzania wakitokea Burundi.UNHCR imegundua kuwa Tanzania inakumbana na mzigo mkubwa kwa kuwahudumia wakimbizi hawa ilhali hawapati fedha za kutosha kuwahudumia wakimbizi na wengine wanaotafuta hifadhi.
    Kambi moja kwa mfano ya Nyarugusu, ambayo inatajwa kuwa ni moja ya kambi kubwa za wakimbizi duniani, inahifadhi wakimbizi 139,0000 idadi ambayo inapaswa kupunguzwa na kuwagawa wakimbizi katika kambi nyingine.
    Hata hivyo serikali ya Tanzania imesifiwa kwa kuendelea kubeba mzigo huu mkubwa wa wakimbizi lakini zaidi kwa kukubali kutekeleza mkakati mpya wa kimataifa ujulikanao kama COMPREHENSIVE REFUGEE RESPONSE.


    Mkakati huu unalenga kutafuta namna endelevu ya kuwasaidia wakimbizi kupata ulinzi na mahitaji mengine ya msingi ya kibinadamu, lakini zaidi sana kutafuta namna ya kuwashirikisha wakimbizi hawa katika shughuli mbali mbali za maendeleo katika nchi wanazokimbilia. 

    No comments:

    Post a Comment