• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Tuesday, 20 June 2017

    Kauzu FC wameshika usukani wa kundi H, Ndondo Cup 2017.

    Ndondo Cup 2017 imeendelea leo kwenye uwanja wa Tandika Mabatini kati ya Kauzu FC dhidi ya Sheraton FC, ambapo Kauzu waliibuka kidedea na ushindi wa mabao 2-1.
    Kauzu walipata bao la kwanza dakika ya 5 mfungaji akiwa ni “Hamad Kibopile” dakika 23 Kauzu wakafunga bao lao la pili likifungwa na “Awadh Said” na kuwafanya Kauzu kwenda mapumziko na akiba ya magoli hayo 2 kwa 0.

    Kwenye kipindi cha pili Sheraton walijipanga na kuongeza kasi katika mchezo kwa kulisakama goli la wapinzani na kufanikiwa kufunga goli dakika ya 56,hivyo kuwafanya wakaambulia goli moja la kufutia machozi na kuwaachia Kauzu pointi 3 muhimu.
    Na game nyingine ilikuwa ni kati ya “ Faru Jeuri” dhidi ya “Miami” kwenye uwanja wa Benjamini Mkapa mchezo ambao umemalizika kwa timu hizo kutoa sare bila kufungana.

    No comments:

    Post a Comment