• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Tuesday, 20 June 2017

    Raisi Dkt John Magufuli ahutubia wananchi wa mkoa wa Pwani siku ya kwanza ya ziara mkoani humo.

    Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli awahutubia wananchi wa mkoa wa pwani maeneo ya kibaha maili moja,kwenye siku ya kwanza ya Ziara yake kwenye mkoa huo,leo hii juni 20 2017.
    Hakika wanachi walionekana kuvutiwa na ziara hiyo ya Raisi Magufuli kwani waliweza kujitokeza kwa wingi,na kuyafanya mapokezi hayo kuwa makubwa lakini pia waliweza kuonesha imani kwa Raisi wao.
    Ameendelea kulia na wale wote wanaotaka kuharibu mali za taifa hili,amewaomba wananchi kuendelea kumuunga mkono kwani kama kero za wananchi hazina vyama,hivyo ili taifa liende mbali ni lazima rasilimali ziangaliwe na kusimamiwa kwa umakini mkubwa ili taifa liweze kujiendesha kiuchumi.
    Japokuwa changamoto ni nyingi,lakini bado tunaendelea kuzimaliza taratibu na tuna uhakika zitamalizika na mambo kuwa sawa ili watanzania wa hali ya chini waendelee kuona mema na neema za nchi hii.na hili najua tutakubaliana kuwa tumeziba mianya ya ubadhilifu,tumeendelea kusimamia wakwepa kodi kulipa ili tuijenge nchi kwa kiwango ambacho katika utawala wa awamu yangu naamini watu watajua kwanini tutaendelea kusisitiza watu kuwa wazalendo.

    No comments:

    Post a Comment