• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Saturday, 24 June 2017

    Mexico imewaliza Waandaaji Confederation Cup Urusi ,Ureno Yatoa dozi kali.

    Michuano ya soka ya mabara imeendelea kushuhudiwa pale nchini Urusi ambapo michezo miwili imepigwa ili kuzipata timu za kuingia nusu fainali.Hatimae wenyeji wa michuano hiyo Urusi wamecheza dhidi ya timu ya Mexico ambapo ilishuhudiwa waandaaji hao wa michuano hiyo kwa mwaka huu wakitupwa nje ya michuano hiyo.
    Mexico waliibuka kidedea kwa ushindi wa mabao 2-1, ingawaje Urusi ndio walitangulia kucheka na nyavu za Mexico katika dakika ya 25 kupitia kwa Aleksandr Samedov kabla ya Nestor Araujo kusawazisha dakika ya 30.

    Kwenye kipindi cha pili Mexico walionekana kuja na kasi nzuri iliyowawezesha kupata bao la ushindi dakika ya 52 kupitia kwa Hirving Lorzano hivyo mchezo ukamalizika wa Mexico kusonga mbele kwenye hatua inayofuata huku wenyeji wakijawa na simanzi.

    Mabingwa wa Ulaya Timu ya taifa ya Ureno waliokuwa wakicheza na vibonde wa Newzealand ambapo Ureno walishusha kipigo cha mbwa mwizi kwa kuinyuka Newzealand bao 4-0.wachezaji walioipatia Ureno ushindi ni “Ronaldo, Bernardo Silva ,Andre Silva, Louis Nani”, Matokeo haya yanazibebe Ureno na Mexico kuelekea nusu fainali kwa kusubiria matokeo ya timu zitakazofuzu hatua hiyo toka kwenye kundi B.

    No comments:

    Post a Comment