• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Thursday, 1 June 2017

    Lava Lava aikubali timu na Familia ya WCB

    Msanii Lava lava amezungumza kwenye kipindi cha Papaso cha TBC Fm, kwa kusema WCB ni familia ambayo inafanya kazi kwa ushirikiano na kuelekezana hivyo suala la kufunikana halipo.

    Wasanii wa WCB wote ni wakali kwenye kazi, tena ukikaa unasema hii sehemu nitapitaje hapa lakini mwisho wa siku kitu ambacho kinanipa moyo ni kwamba hadi umeona uongozi umekaa na kuamua kunitoa mimi kunipeleka mbele za watu ujue kuna kitu kwangu. Msanii yeyote wa WCB nipo tayari kufanya nae kazi… kufunikwa ni sehemu ya kujipima, ila mwisho wa siku kila mtu ana mashabiki wake,” aliongea Lava Lava


    Lava Lava ambaye anakamilisha idadi ya msanii wa tano kujiunga na Lebo ya WCB ambapo wengine waliotangulia ni Harmonize, Rayvanny, Queen Darleen na Rich Mavoko.na msanii huyu amekuja vizuri kwenye muziki kwani Wimbo wake wa kwanza kutoa unaitwa Tuachane unafanya vizuri sana kwenye media kwa sasa.

    No comments:

    Post a Comment