• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Thursday, 1 June 2017

    Dkt Magufuli amepata dawa ya wanaokwepa kodi nchini Tanzania.

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DtkJohn Pombe Magufuli amesema kuanzishwa kwa mfumo mpya wa serikali wa ukusanyaji kodi kwa njia ya Kielekroniki, (Data Center) itakuwa dawa kwa wote wanaokwepa kulipa kodi.
    Ameyaongea haya alipokuwa akizindua uanzishwaji wa mfumo huo,ambapo pia anaamini mfumo huu utasaidia kuondoa malalamiko ya wale wanaodai kubambikiziwa kodi isiyo na uwiano,lakini hata wale wanaokwepa kulipa kodi ufumbuzi ni huu wa kuwepo kwa kituo hicho.pia amesisitiza wafanyabiashara na makampuni kuingia katika mfumo huu ili kukwepa udanganyifu kwa ustawi wa nchi.
    Lengo la kuanzishwa kwa kituo hicho ni dhamira ya serikali ya Tanzania katika kukuza na kuimarisha sekta ya Teknolojia na Habari na mawasiliano ambayo inakuwa kwa kasi ulimwenguni kote na ni kichocheo kikubwa cha uchumi.lakini kudumisha muungano ni sehemu ya mpango huo kwani tozo zote zitakuwa wazi katika kutanabaisha walipa kodi kwa pande zote mbili Jamhuri ya muungano wa Tanzania.

    No comments:

    Post a Comment