• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Wednesday, 31 May 2017

    Reli mpya ya kisasa yazinduliwa huko nchini Kenya.

    Kenya imezindua reli mpya kati ya mji wa Mombasa hadi Nairobi,Reli hiyo imetengezwa kwa ufadhili wa toka serikali ya China.

    Mradi huo mkubwa kimiundombinu umechukua takriban miaka mitatu na nusu kwa kutumia teknolojia ya ujenzi wa reli ya China,Reli hiyo inatarajiwa kuunganisha Sudan Kusini, DR Congo ,Burundi na Mombasa.
    Safari ya kutoka Mombasa kuelekea Nairobi na treni ya kisasa itachukua saa nne na nusu ikilinganishwa na saa tisa kwa kutumia basi na saa 12 kwa kutumia treni ya zamani.Nauli ya watu watakaokalia viti vya kawaida ni shilingi 900 huku wale watakaosafiri kwa kutumia business class wakilipa shilingi 3,000.
    Serikali ya kenya imeendelea kuimarisha miundombinu katika kuhakikisha wanawavutia wawekezaji wengi kuja kuwekeza nchini humo,ambapo wameendelea kuamini Madaraka Express itawasaidia katika kufikia malengo muhimu.

    No comments:

    Post a Comment