• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Wednesday, 31 May 2017

    IGP mpya Simon Sirro ameongea na waandishi wa habari Jijini Dar es salaam.

    Ameanza kwa kuwashukuru waandishi wa habari kwa kutenda kazi zao vizuri,kwa habarisha watanzania,ameomba kuendeleza ushirikiano waliouonesha hapo awali kwa Igp aliyepita,amemshukuru Rais kwa kumteua katika nafasi hiyo.

    Ameeleza hali ya usalama nchini bado iko sawa,japo kuna maeneo machache kama rufiji ambapo amesema hatotaka kuzungumza bali majibu yatapatikana.

    " Salamu kwa hilo kundi la watu wachache,ambao wanatengeneza na kufanya mabaya basi ubaya wao utarudishwa kwa ubaya wa kisheria zaidi".

    "Ameeleza kuwa kundi la bodaboda ambao wamee,ambao wameanza kufunja sheria kwa makusudo waache mara moja,ameonya pia watu wanaojiita wenye hasira kali kwa kuwaadhibu watu pindi wawakamatapo kwa kigezo cha hasira kali".

    "Wote tunajua kuwa rushwa ni adui wa haki,maelekezo yameshatoka kwa watu wote wanaopenda kutoa rushwa,wataziacha familia zao".

    "Pia amesema kama kuna mtu atakaetoa taarifa za uhakika,juu ya wale wanaosumbua kibiti na amesema majibu yatapatikana ndani ya muda mfupi,amesema hakuna safu mpya atakayokuja nayo bali polisi ni walewale na anaamini atashirikiana nao vizuri sana kuhakikisha usalama unaimarika".

    "Amemalizia kwa kusema iwapo askari amekufa kwenye mapambano ,hiyo ni ajali kazini na amesema atapenda matendo yazungumze dhidi ya vitendo kwa kuwahakikishia watu wa pwani usalama ulio sahihi kwa kushirikiana".

    "Kazi ya upelelezi haina muda maaalumu lakini, wananchi wasubiri majibu mazuri hasa walio raia wema,walio raia wema hawana sababu ya kukimbia na tutaenda kuzungumza nao muda si mrefu,bali waliofanya mambo maovu lazima wakimbie mapema sana".

    No comments:

    Post a Comment