• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Wednesday, 31 May 2017

    Mwenyekiti wa kambi rasmi ya upinzani bungeni,Freeman Mbowe amethibitisha taarifa za kifo cha mzee Ndesamburo.


    Leo Mei 31, 2017 majira ya mchana kwa saa za hapa Tanzania zilisambaa taarifa ambazo zilikuwa zinaeleza kifo cha aliyewahi kuwa Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo.

    Hivyo baada ya kuenea kwa habari hizo,Mwenyekiti wa Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni Mh “Freeman Mbowe“amekutana na Waandishi wa Habari Dodoma ili kutoa uthibitisho huo.

    Ameeleza amependa kuthibitisha kuhusu habari zinazoendelea kusambaa za kifo cha Mzee Ndesamboro,amesema ni kweli tukio hilo limetokea,na hivi karibuni alikuwa mjini Dodoma,ambapo baada ya kurejea Moshi na kufanya mazungumzo na wadau kadhaa akiwemo meya wa Arusha kwa lengo la kuweza kutoa rambirambi kwa tukio la wahanga wa ajali ya Luck Vincent.

    “Imeelezwa kuwa alipoanza kuandika check,ya rambirambi hiyo ndipo akaanza kupoteza nguvu,ambapo walimkimbiza hospitali wakishirikiana na wanafamilia,na baada ya mda kiasi ndipo madaktari walikuja na kueleza kuwa mzee wetu amepoteza maisha.”


    “Hakika chama kimepoteza mtu shujaa,na wa muhimu mno.hivyo kwa kutambua mchango wake,tutawajulisha watanzania wote kupitia vyombo vya habari tofauti na hata kwa kutumia mitandao ya kijamii ili taarifa hii iwafikie watanzania wengi zaidi”.

    No comments:

    Post a Comment