• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Wednesday, 21 June 2017

    Bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania limepitisha,Bajeti kuu ya serikali kwa mwaka 2017/2018

    Mbunge wa Jimbo la Mtama, Mhe. Nape Mnauye akimpongeza Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), kwa kufanikisha kuandaa Bajeti ya kihistoria ya shilingi trilioni 31.7 ya Mwaka wa Fedha 2017/2018,iliyopitishwa mjini Dodoma
    Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako (Mb), akimpongeza Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), kwa kufanikisha kuandaa Bajeti Kuu ya Serikali ya kihistoria ya shilingi trilioni 31.7 ya Mwaka wa Fedha 2017/2018.
    Mbunge wa Jimbo la Misungwi, Mhe. Charles Kitwanga akimkumbatia kwa furaha,Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), kwa kufanikisha kuandaa na hatimaye kupitishwa kwa Bajeti ya kihistoria ya shilingi trilioni 31.7 ya Mwaka wa Fedha 2017/2018.
    Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kushoto), akiteta kidogo na maafisa waandamizi wa Wizara yake nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma, baada ya Bunge kupitisha kwa kishindo Bajeti Kuu ya Serikali ya shilingi trilioni 31.7. 

    No comments:

    Post a Comment