• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Tuesday, 2 May 2017

    Rais Magufuli na serikali ya awamu ya tano yaahidi kupandisha mishahara,kupandisha vyeo na promosheni kwa wafanyakazi wake wa Umma.


    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli leo Mei mosi, 2017 amehutubia kwenye maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani iliyofanyika kitaifa katika Viwanja vya Ushirika Moshi, mjini huko mkoani Kilimanjaro

    Rais Magufuli ameeleza ni muhimu tukaendelea kujenga uchumi wa Tanzania mpya,ameahidi serilkali kuongeza onezeko la kawaida la mshahara na huku promosheni zikizingatiwa kwakuwa zoezi la kusafisha nyumba iliyokuwa imejaa uchafu limekamilika


    Pamekuwa na matatizo mengi sana ya udanganyifu mwingi,amesisitiza kuwa patakuwepo na kulipwa kwa malimbikizo,sambamba na ongezeko la mshahara lakini pia ameahidi kutoa ajira takribani 52,000 kikubwa wafanyakazi wote kwa ujumla tunapaswa kulinda amani,kupambana na janga la madawa ili kuwa na taifa lenye vijana wanaojitambua na kuongeza uzalishaji kwa kuzingatia vipaumbele vya serikali kuelekea kwenye uchumi wa viwanda.

    No comments:

    Post a Comment