• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Tuesday, 2 May 2017

    Mei mosi ilivyojiri na maandamano makubwa huko Venezuela .



    Siku ya mei mosi ambayo ni siku ya wafanyakazi duniani ilikuwa na changamoto katika nchi ya Venezuela ambapo zilizuka vurugu na maandamano miongoni mwa wananchi kumpinga rais wa Venezuela Nicolas Maduro kwa kile alichoeleza kwenye hotuba yake.

    Rais Maduro, alipendekeza liundwe Bunge la katiba ambalo litakuwa na mamlaka ya kuandika katiba mpya,kwa madai kuwa chombo hicho kipya kitaundwa na raia wa kawaida,na kuachana na bunge la kitaifa linaloonekana kuwa na wapinzani wengi.

    Kwa upande wa kiongozi wa Upinzani, nchini Venezuela, Henrique Capriles amesema chombo hicho kipya kitakuwa kina malengo ya kuhujumu katiba .Na mara kdhaa imeonekana Bunge la kitaifa likitaka Rais Maduro ajiuzulu kutokana na taifa hilo kuendelea kukabiliwa na hali mbaya na isiyoridhisha kiuchumi

    No comments:

    Post a Comment