• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Wednesday, 3 May 2017

    Dr Kigwangala na taarifa ya kuimarika kwa upatikanaji wa dawa nchini.

    Naibu Wazara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia,Wazee na Watoto, Dr Hamisi Kigwangala amesema kuwa hali ya upatikanaji wa dawa nchini sasa imeimarika na kufikia asilimia 83 ambapo ameishukuru serikali ya awamu ya tano kwa kuendelea kuboresha huduma za afya kwa wananchi wake.

    Ameongeza kuwa kwa Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Mheshimiwa John Pombe Magufuli,upatikanaji wa dawa ni kipaumbele na kuimarisha idara ya afya kwa ujumla,kwa kuboresha huduma kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya kwa umma kote nchini.
    Katika kuhakikisha haya yamawezekan serikali ya Awamu ya Tano ilichukua jitihada za haraka na za lazima kwa kuongeza bajeti ya dawa kutoka shilingi Bilioni 31 kufikia shilingi Bilioni 251.5.ambapo ongezeko hilola fedha hizo zimeimarisha hali ya upatikanaji wa dawa nchini,jumla ya Bilioni 112 zilikwisha kutolewa na kupelekwa Bohari ya Dawa ili kuviwezesha vituo vya kutolewa huduma za Afya vya Umma kupata mahitaji yake ya Dawa,Vifaa,Vifaa tiba pia.alimalizia” .Dr Kigwangala


    SapulaMedia android app sasa inapatikana playstore: Kwa kupata Habari za karibu kuhusu:\\ Habari, Muziki na burudani,Michezo,Technolojia,Ujasiriamali ili kupakua bonyeza link --->>>


    No comments:

    Post a Comment