• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Friday, 28 April 2017

    Waziri wa sanaa,utamaduni na michezo, Dkt Mwakyembe apewa tuzo na RITA.

    Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini nchini (RITA), umempa Tuzo, aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria Dkt Harrison Mwakyembe, kwa kutambua mchango wake katika kuboresha hali ya usajili wa matukio muhimu ya binadamu nchini
    Dkt Mwakyembe amekabidhiwa Tuzo hiyo na Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi, katika Ofisi za Wizara mjini Dodoma.
    Kwa upande wa Profesa Kabudi, amempongeza Dkt Mwakyembe kwa jinsi alivyojitoa na kuhakikisha hali ya usajili inaboreshwa na hivyo kuinua muamko wa wananchi na kuona umuhimu wa kujisajili na kuwa na cheti cha kuzaliwa.

    Dkt. Mwakyembe baada ya kupokea Tuzo hiyo alisema “Sina neno kubwa la kuwaambia zaidi ya Kushukuru kwa kusema asante”. “Asanteni sana, niwaahidi kwamba nitaendelea kuwaunga mkono huko nilipokwenda. Nanyi lazima muendeleze kazi ya kuhamasisha usajili kwa nguvu zenu zote, na mjue kwamba mna kazi kubwa mbele yenu na ni lazima ifanikiwe.”

    No comments:

    Post a Comment