• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Friday, 28 April 2017

    Mbunge wa Bariadi Andrew Chenge amedai kuwa ataiomba serikali iache maneno na kuweka muziki.


    Mbunge wa Bariadi Andrew Chenge amesema atalazimika kuiambia serikali iache maneno baaya ya kuwa imepita muda mrefu hadi sasa ikiahidi kufanya ujenzi wa barabara katika jimbo lake huku utekelezaji ukichukua muda mrefu.

    Aidha amesema anaipongeza serikali ya awamu ya tano,ambayo imeendelea kuunganisha nchi yetu kwa miradi ya barabara nyingi na zinazopitika ambazo baadhi zimekamilika na nyingine,zinaendelea kukamilika.

    Aliendelea kuiomba serikali kuunganisha barabara itakayo unganisha singida na simiyu kupitia iguguno,na wilaya ya mkalama singida,mpaka kuifikia bariadi,na kuangalia pia barabara ambayo itaunganisha simiyu na arusha.


    Chenge alimalizia kwa kusemaKwa mwaka huu nakubaliana na serikali kuhusu madai yao kwamba wamekamilisha upembuzi kuhusu ujenzi wa barabara jimboni kwangu, mwaka kesho kama ikiendelea hivi mimi nitasema waache maneno waweke muziki

    No comments:

    Post a Comment