• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Friday, 28 April 2017

    Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi Bora Mhe. Angellah Kairuki amebainisha kundi lililopitiwa na sakata la vyeti feki.

    Waziri Kairuki amebainisha hayo leo katika ukumbi wa Chimwaga uliopo ndani ya Chuo Kikuu cha Dodoma, wakati anatoa taarifa ya uwasilishaji wa uhakiki wa vyeti feki kwa watumishi wa umma,lilioendeshwa na Serikali kuanzia mwezi Oktoba mwaka 2016.

    Zoezi hili la uhakiki wa vyeti feki kwa watumishi wa umma liliwahusisha watumishi wa umma pekee wakiwemo makatibu wakuu,watendaji na maofisha wengine mbalimbali wa ngazi za serikali, zoezi hili halikuwahusisha viongozi wa kisiasa” alisisitiza waziri Kairuki.
    Watumishi 9,932 wamebainika kuwa na vyeti vya kughushi sawa na asilimia 2.4, Wenye vyeti vyenye utata ni 1,538 vilikuwa vikitumiwa na jumla ya watu 3,076, wenye vyeti halali pekee ni asilimia 94.23. Hatua zitachukuliwa kwa wenye vyeti feki pamoja na,bali hata kwa wahusika waliotengeneza vyeti hivyo”.
    Waziri Kairuki alimaliza kwa kusema wale wote wanajijua wanatumia vyeti vya kughushi waache mara moja, kwa kuwa ni kosa la jinai huku akisisitiza kuwa adhabu yake ni kufungwa jela miaka saba.


    No comments:

    Post a Comment