• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Wednesday, 5 April 2017

    Waziri mwakyembe azungumza juu ya TRA kuchukua gari la serengeti boys.

















    Waziri mwenye dhamana ya michezo Dr. Harrison Mwakyembe azungumza baada ya taarifa ya kwamba timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’ ilishushwa kwenye mabasi na TRA wakati ipo njiani kwenda kwa makamu wa Rais mama Samia Suluhu Hassani ambaye aliialika timu hiyo nyumbani kwake.
    Mwakyembe amesema ni aibu kwetu kama taifa hasa kwa kipindi hiki ambacho watanzania tunapaswa kuunganisha nguvu zetu katika kuhamasisha michezo na kuwatia moyo wachezaji wetu ili timu ifanye vizuri na sio kukwamisha jitihada za kuinua michezo kote nchini.
    Vijana wetu walikuwa wanakwenda kwa kiongozi wetu kwa mwaliko, lakini basi lao likasimamishwa na watu wa TRA kisha wakaondolewa kwenye mabasi na magari kuchukuliwa, ikabidi viongozi wa TFF waanze kutafuta magari mengine, ili kukamilisha safari hiyo”
    Aidha waziri Mwakyembe amewaomba TRA kuendelea kufanya kazi yao kwa mujibu lakini pia kutumia busara pale inapobidi.
    Baada ya tukio hilo,Waziri mwakyembe amemwagiza katibu mkuu wake kukaa na katibu mkuu wa Wizara ya Fedha na viongozi wa TRA kwa pamoja,ili kuepusha aibu za namna hii kwa wakati mwingine.
    Nasema kwa masikitiko kwa sababu timu hii ilipoanza nilikuwa nawafuatilia sana, mechi yao ya kwanza ilibidi wasafiri hadi Kigoma kwa basi kwa sababu akaunti za TFF zilifungwa, wakafika Kigoma wakiwa hoi kwa safari ndefu ikabidi waiombe timu ya Burundi kuja Kigoma kucheza nao, wakafungwa 2-1. Sasa leo basi lao linakamatwa wakati tupo kwenye kampeni ya kitaifa kuhakikisha vijana wanafanya vizuri na kuliletea sifa taifa”.
    Baadae usiku, ilitoka taarifa kutoka kwa afisa habari wa TFF Alfred Lucas kwamba, kampuni ya udalali ya Yono ambayo ni wakala wa TRA imetangaza kuliachia mara moja basi ambalo linatumiwa na Serengeti Boys.



    No comments:

    Post a Comment