• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Friday, 7 April 2017

    vyombo vya dola na ufafanuzi wa kupotea kwa msanii Roma mkatoliki na wenzake.

















    Chombo cha dola kimendelea kutoa ufafanuzi,juu ya taarifa za tukio la kupotea kwa Msanii wa Bongo Fleva hapa nchini, “Ibrahim Mussa” maarufu kwa jina la “Roma Mkatoliki” na wenzake,pia kuendelea kuwaomba wasanii na wananchi kwa ujumla kuendelea kuwa watulivu katika kipindi hiki.


     Aidha kimendelea kusema kwa yeyote atakayepata taarifa zitakazosaidia katika upelelezi wa tukio hili atoe ushirikiano kwenye vyombo vya dola mapema.

    Haya yamesemwa na kamanda wa polisi kanda maalumu Dar es salaam Simon Sirro,na hii ni baada ya kutokea kwa tukio hilo mapema hii,hivyo basi amesisitiza kuwa Jeshi la Polisi limeendelea na hatua za kipelelezi wa tukio hilo mapema baada ya taarifa kuwafikia.

    Ameongeza kwa kuwaomba baadhi ya watu kutokuwa wepesi wa kusambaza uvumi pasipokujua uhalisia au undani wa jambo kabla hawajaliongelea.

    unajua mambo ya uvumi sio mazuri,kikubwa tuviachie vyombo husika vifanye kazi yake na kuvisaidia pale inapobidi” alisisitiza kamanda Sirro.


    No comments:

    Post a Comment