• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Thursday, 13 April 2017

    Watu wapatao 90 au zaidi wahofiwa kuzama baharini huko llibya


    Zaidi ya watu 90 wanahofiwa kufa maji huko pwani ya libya,ambapo inasemekana mashua ambayo inakadidriwa kubeba wahamiaji 120 ilizama,shughuli za uokoaji bado zinaendelea.
    Njia hizo za baharini zimekuwa zikitumiwa na wahamiaji na wakimbizi wengi kuingia kusini mwa Ulaya kutafuta hifadhi, Aidha msemaji wa kikosi cha ulinzi pwani ya mji wa Tripoli “Ayoub Kassem”, amesema anaamini kuwa kila mtu ambaye alikuwa katika mashua hiyo alitoka nchi za kusini mwa jangwa la sahara.
    Watu 23 kati ya watu 120 waliokolewa baharini,na wamepelekwa kwenye hifadhi na uangalizi na walieleza kuwa kati ya waliozama kuna kundi la watoto na wanawake.


    No comments:

    Post a Comment