• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Wednesday, 12 April 2017

    Taiwani yapiga marufuku ulaji wa mbwa na paka







    Bunge la Taiwan, limeidhinisha mswaada wa kupiga marufuku uchinjaji wa paka na mbwa, kwa matumizi ya binadamu.
    Mswaada huo pia umepiga marufuku wale wanaotumia gari au pikipiki kuwavuta wanyama wao wa kuchezea, au kuwatanguliza wanaposafiri,na atakayepatikana akienda kinyume, atakabiliwa na faini kubwa au kufungwa hadi miaka miwili jela na majina na picha zao kuwekwa hadharani.
    Hatua hiyo imeanzishwa ili kuboresha sheria za kuwalinda wanyama nchini Taiwan, na ni moja ya aina yake kuanza kutekelezwa barani Asia.

    Mwaka 2001, Taiwan ilipitisha sheria ya kupiga marufuku uuzaji wa nyama na manyoya ya wanyama wa kuchezea kama vile paka na mbwa, kwa kile kilichotajwa "madhumuni ya kiuchumi". Nyama ya mbwa, zamani zilitumika kama chakula, lakini kwa sasa mnyama huyo anafaa kujumuishwa kama mmojawepo wa wanafamilia.

    No comments:

    Post a Comment