• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Friday, 21 April 2017

    Watu saba wafariki wakiangalia mchezo kati ya Manchester United nchini Nigeria

    Nchini Nigeria watu saba walifariki dunia na wengine kujeruhiwa baada ya kutokea hitilafu kwenye mfumo wa umeme walipokuwa wakitazama mchezo kati ya Manchester United na Anderlecht.

    Mashabiki hao wa soka waliokuwa wamekusanyika kwenye eneo lililokuwa likitumika kuonesha mechi hiyo kupitia runinga huko kwenye mji wa Calabar.katika mchezo huo “Manchester United” walishinda 2-1 kwenye mechi hiyo ya hatua ya robofainali ligi ndogo ya klabu Ulaya, Europa League.

    Polisi nchini Nigeria wamesema watu saba walifariki na wengine takribani 10 wakajeruhiwa na wamelazwa hospitalini.inasemekana chanzo cha tukio hilo ni kuanguka kwa waya mkubwa unaopitisha umeme kwenye jumba hilo.

    maafisa wa polisi walieleza kuwa, "watu 7 walikuwa wamefariki na wengine10 wamelazwa hospitalini na mmoja mmoja kati yao yupo chumba cha wagonjwa mahututi"

    No comments:

    Post a Comment