• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Friday, 21 April 2017

    Celta vigo kiboko ya Genk yaangukia kwa mashetani wekundu"Man united".

    Baada ya kuwachakaza Genk, klabu ya Celta Vigo itakutana uso kwa uso na Manchester United katika hatua ya nusu fainali ya michuano ya Europa League.

    United ambao msimu huu hawana uhakika wa kuingia katika top four ya ligi kuu Uingereza wanalazimika kufanya kazi kubwa kwenye mashindano ya Europa kwani wakishinda kombe hilo watafudhu Champions League kama mabingwa wa Europa.

    Celta Vigo ina wakati mgumu wa kuhakikisha mbio za man u,hazifiki mbali ijapokuwa man United, nao wanapaswa kuwatazama Celta Vigo kwa jicho la tatu kwakuwa wana rekodi nzuri katika mechi zao za ugenini za Europa msimu huu.


    Nusu fainali ya michuano hiyo inatarajia kupigwa tarehe 4 mwezi ujao, kabla ya timu hizo kurudiana tarehe 11 mwezi huo huo wa tano.

    No comments:

    Post a Comment