• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Friday, 21 April 2017

    Nikki wa Pili atoa ushauri huu kwa wasanii wa bongo movie.

    Ikiwa ni siku chache tu baada ya mastaa wa Bongo movie kulalamikia wakitaka filamu za kigeni zizuiliwe nchini,watu malimabali wametoa maoni yao juu ya jambo hilo na hata wengine kukosoa uamuzi huo.

    Miongoni mwa watu waliotoa maoni yao juu ya ishu hii ya Bongo movie ni Nikki wa pili toka Weusi,ambaye amefunguka kupitia Twitter akaunti yake ametoa maoni yake kwa wasanii wa bongo movie kuwa wanatakiwa wafahamike zaidi kwenye movie zao ili kulinda kazi zao kama wafanyavyo wasanii wa nje.

    “Movies za rambo ni maarufu kuliko rambo mwenyewe, bongo movies tunawajuwa kwa vitu vingine zaidi wala hata sio movie zao.Ni kweli tunahitaji kulinda soko la ndani, la movies lakini wao wanahitaji kufanya tafakuri ya kina.

    “Bongo movies mwanzoni walikuwa na soko, kuanza ni kujaribu, but ku sustain is a science… mwendelezo wa lolote huitaji maarifa.Nchi zote zilizoendelea zililinda masoko ya nyumbani, ndio tulilinde lakini wenye movie nao wajilinde kwa kujiongeza kila kukicha.” 

    Ameandika “Nikki wa Pili”.

    No comments:

    Post a Comment