• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Thursday, 27 April 2017

    Vyama vya Upinzani Kenya vyamteua Raila Odinga kuwa mgombea Urais.

    Muungano wa vyama vya upinzani nchini Kenya National Super Alliance (NASA) wamemteua Raila Odinga kuwa mgombea kwa tiketi ya umoja huo kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Agosti mwaka 2017.

    Bw Odinga sasa atakabiliana na Rais Uhuru Kenyatta atakayetumia chama cha Jubilee kuwania muhula wa pili.“Hii ni heshima kubwa sana ambayo ndugu zangu wamepatia, kwa kuniweka nipeperushe bendera ya NASA.Tumekuwa na vikao ambavyo vimechukua siku nyingi. Kila kitu tumeandika, tumekubaliana ya kwanza serikali tutakayoiunda, ambayo ni serikali ya mseto itakuwa ni serikali ya mpito,” ni maneno ya Odinga alpokuwa akihutubia baada ya kutangazwa kuwa mgombea.

    Alisema serikali yake itaangazia kumaliza umasikini, kuimarisha afya, kuboresha uchumi, kubuni nafasi za kazi na kurejesha gharama ya elimu na maisha chini,Aidha Odinga ameahidi kuhakikisha walimu na madaktari,pamoja na wafanyakazi wengine wanalipwa mishahara mizuri bila kusahau kutokomeza vitendo vya rushwa.


    No comments:

    Post a Comment