• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Friday, 28 April 2017

    Naibu waziri wa mambo ya ndani nchini Tanzania ametoa ufafanuzi bungeni kwenye maswali aliyoulizwa kwa kusema haya.

    Naibu Waziri wa mambo ya ndani ya nchini Tanzania Eng Hamad Masauni amesema kumekuwa na matukio kadhaa ya Jeshi la Polisi, waandishi wa habari pamoja na wananchi wa kawaida kufanyiwa fujo na baadhi ya watu hivyo serikali itahakikisha inachukua hatua kali za kisheria kwa watuhumiwa.

    Eng. Masauni amesema”Uhalifu wa aina yoyote utakaofanywa na mtu au chama chochote dhidi ya raia yeyote hatutokubali na tutachukua hatua kali za kisheria”

    maeneo yamkuranga,kibiti, na rufiji ni sehemu ambayo inaangaliwa kwa jicho la tatu na tumejitokeza maeneo hayo kuwaomba wananchi wasaidiane na jeshi la polisi kwa kujenga mahusiano mazuri ili kusaidiana kupata taarifa za wahalifu”

    Serikali inajipanga kufikisha huduma za upatikanaji wa leseni na miundombinu,kwa wananchi wa eneo la Tarime Rorya,aidha tunatarajia kufikisha huduma kwenye mikoa yote mipya na maeneo ambayo huduma za utoaji leseni,na kujenga miundombinu kulingana na bajeti yetu.”

    Alimaliza kwa kusema ili sheria isiweze kukukumba,ni vyema ukaishi kwa kufuata sheria na kanuni na si vinginevyo.


    No comments:

    Post a Comment