Wawakilishi
pekee wa Tanzania kwenye mashindano ya kimataifa, Yanga SC wamepata
ushindi wa goli 1-0 dhidi ya MC Aalger mchezo uliochezwa leo kwenye
uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam.
Japo wageni wa Yanga waliendelea kutumia mbinu za kimpira za ukanda wa Kaskazini mwa Afrika,kwa wachezaji wa MC Alger kujiangusha angusha na kupoteza muda lakini bado mambo yaliwawia ngumu na mchezo kumalizika kwa Yanga kutoka kifua mbele kwa goli 1-0.
Goli
hilo la Yanga limefungwa na kiungo "Thabani Kamusoko" dakika ya 61 alipopewa pasi na Chirwa karibu na eneo 18 upande wa
goli la MC Alger, Kamusoko hakufanya ajizi na kuitumia nafasi
aliyoipata kuwapa burudani mashabiki.
Mshambuliaji
Donald Ngoma aliongeza nguvu kwenye safu ya ushambuliaji ya Yanga
akisaidiana na Obrey Chirwa ambaye alikuwa kwenye kiwango kizuri
kwenye mchezo wa leo licha ya kukosa nafasi kadhaa.
Japo wageni wa Yanga waliendelea kutumia mbinu za kimpira za ukanda wa Kaskazini mwa Afrika,kwa wachezaji wa MC Alger kujiangusha angusha na kupoteza muda lakini bado mambo yaliwawia ngumu na mchezo kumalizika kwa Yanga kutoka kifua mbele kwa goli 1-0.
No comments:
Post a Comment