• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Saturday, 22 April 2017

    Tanzania prison yapokea kipigo cha goli 3-0 toka kwa wana janwani,Yanga

    Mabingwa watetezi wa kombe la shirikisho (FA) Yanga, wametinga hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Tanzania Prisons,ambapo mchezo ambao umefanyika katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam,kwa sasa yanga inaungana na timu za Simba, Azam na Mbao FC katika hatua ya nusu fainali ambapo droo inasubiriwa.
    Tanzania Prisons kwenye mchezo wa leo walipata penalti dakika ya 54 lakini mpigaji Victor Hangaya aligongesha mwamba,Baada ya ushindi huo, Yanga inakamilisha timu nne za nusu fainali, droo ya hatua hiyo itafanyika siku ya kesho tarehe 23 april,2017 ili kuzitambua timu zitakazokutana nusu fainali.

    No comments:

    Post a Comment