• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Monday, 24 April 2017

    Studio ya Tongwe recods walipotekwa Roma na wenzake yafungwa kwa muda.


    Ni wiki kadhaa zimepita tangu “Roma Mkatoliki” na wenzake watatu, Moni, Imma na Bin Laden, walipotekwa wakiwa kwenye Studio ya Tongwe Records iliyopo Masaki, habari zilizopo kwa sasa kwamba studio hiyo imefungwa na haifanyi kazi kwa sasa.

    J Murder wa tongwe records amedai studio hiyo itafunguliwa mara tu baada ya mambo kukaa sawa.
    Ni kweli Studio kwa sasa haifanyi kazi kwa sababu watu bado hawajakaa sawa, wanahitaji kupunzika kwanza,” alisema Murder. “Mimi nadhani kwa sasa afya ya vijana wetu ndio kipaumbele cha kwanza, mambo yakitulia kila kitu kitakuwa wazi,”


    Tumeamua kupumzika kwa muda wakati vijana wakituliza akili ili kila mmoja aweze kurudi katika hali yake ya kawaida na kwa waliopata majeraha waweze kupona kabisa,pia ni muda ambao wenzetu jeshi la polisi wanaendelea na uchunguzi wa tukio zima.


    No comments:

    Post a Comment