• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Monday, 24 April 2017

    Mwaka 2017 na kuimarika kwa utalii nchini Tanzania ambapo hifadhi ya mbuga ya Serengeti na bonde la Ngorongoro kuonekana kuwavuta watu duniani kote.

    Mwaka 2017 na kumiminika kwa watalii Tanzania ambapo mastaa na watu mashuhuri wameweza kuzulu kwa lengo la kutalii nchini,ambapo watu kama mwigizaji maarufu wa filamu kutokea Hollywood nchini Marekani,”Will Smith na mkewe Jada Pinkett-Smith” pia mwanamitindo na mrembo, Chanel Iman,aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Taifa la Israel, Bw. Ehud Barak,kwa nyakati tofauti waliweza kutembelea mbuga ya wanyama ya serengeti na vivutio vingine kama hifadhi ya taifa ya ngorongoro.
    Ngorongoro huendwa zaidi kwakuwa ina historia kubwa sana na watu tofauti hupenda kuifuatilia historia hiyo na kutazama mandhari ya kuvutia,lakini pia kwakuwa ndani ya hifadhi hii kabila la wamasai limejikita humo na kuendeleza maisha pasipo kuleta athari kwa wanyama pori waliomo humo.
    Masalia ya Kale ya Binadamu wa Mwanzo. Ngorongoro ndimo linapopatikana bonde la Olduvai ambalo kwa mujibu wa wanahistoria yanapatikana masalia ya binadamu wa mwanzo kuishi duniani. Hapa ndipo wanaikolojia maarufu Dkt. Louis na mkewe Mary Leakey walipata masalia ya kale likiwemo fuvu la mtu wa kale zaidi, Zinjanthropus, ambaye alipata kuishi miaka milioni 1.75 iliyopita. Utafiti wao uliweza kuvumbua mabadiliko ya taratibu ya ukubwa wa ubongo na zana zao za mawe walizokuwa wanazitumia.
    Maziwa kama Ziwa Ndutu na Masek,mlima Oldonyo Lengai ulio nje kidogo ya hifadhi amabo una uasili wa kuwa na volkeno,pia kuna ndege wa aina tofauti kama flamingo ambao wanazidi kuleta mvuto wa pekee.
    Mtu yeyote kutoka pande yoyote ya dunia hii anaweza kufanya utalii na kujionea ,vivutio vingi vipatikanavyo ndani ya hifadhi hii ya ngorongoro,lakini pia kuna sehemu nyingi sana ambazo utajionea mengi ya kustaaajabisha na kukuvutia,mimi na wewe tunaweza kufika kwenye maeneo haya na tukawa mabalozi wazuri kwa wengine kwenye maeneo tutokayo.


    No comments:

    Post a Comment