• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Monday, 24 April 2017

    Mbunge wa viti maalumu Songwe awashangaa wabunge hawa.


    Mbunge wa viti maalum CCM katika mkoa wa Songwe “Juliana Shonza” amesema anawashangaa baadhi ya wabunge ambao mara kwa mara wamekuwa wakisimama bungeni na kwenye majukwaa wakisema kuwa serikali haijafanya kitu kwa ajili ya wananchi wake.

    Haya ameyasema alipokuwa bungeni na alipokuwa anachangia juu ya bajeti ya Tamisemi,akisema baada ya kutolewa kwa elimu bure,idadi ya udahili wa wanafunzi kwa elimu za shule ya msingi umeongezeka na hata pia wanafunzi waliokuwa wanarubuniwa kwa sasa mambo yamebadilika.

    Amesisitiza kwa kusema ,kikubwa ni ushirikiano baina ya viongozi wote wanaowatumikia wananchi,walimu wapewe motisha ili kuweza kufanya kazi kwa moyo na kwa uzalendo kabisa,ameiomba serikali isiishie kuwapa motisha walimu wakuu pekee bali kuwawezesha walimu wote kwa kuwapa motisha itakayowapa nguvu na moyo zaidi katika uendaji kazi na kulitumikia taifa.

    No comments:

    Post a Comment