• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Tuesday, 25 April 2017

    Siku ya malaria duniani,na mpango wa kumaliza ungojwa huo ifikapo mwaka 2030 kote ulimwenguni.


    Chanjo ya kwanza ya malaria duniani itajaribiwa kusambazwa mwaka ujao na imewekwa kipaumbele katika nchi kama Ghana, Kenya na Malawi kuanzia mwaka ujao,WHO limesema chanjo hizo zinaweza kuokoa maisha ya maelfu ya watu,ambapo mpango huo ambao uko katika majaribio utahusisha zaidi ya watoto laki saba wenye umri kati ya miezi mitano na mwaka mmoja na nusu.
    Tafiti mbalimbali zimeshafanywa juu ya kuweza kumaliza tatizo la ugonjwa huu,na zinaonekana kuzaa matunda kila uchwao,chanjo hiyo inayotarajiwa,itaenda sambamba na mbinu mbadala zinazoendelea kutumika kwa kujikinga na malariakama vile neti, dawa za kufukuza mbu, na dawa za kukinga malaria.

    No comments:

    Post a Comment