• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Friday, 14 April 2017

    Shirikisho la soka duniani -FIFA na la Afrika - CAF wameupitisha uwanja wa CCM Kirumba wa jijini Mwanza, kutumika kwenye mechi za kimataifa.

    Rais wa shirikisho la soka Tanzania, TFF, Jamal Malinzi,ampost kwenye mitandao ya kijamii na kusema. “hongereni wana mwanza kwani Uwanja wa CCM Kirumba umepitishwa na CAF na FIFA kutumiwa kwa mechi za Kimataifa,” ametweet Malinzi.

    Hii imekuja baada ya wataalamu wa Ufundi wa CAF kuzulu Mwanza na kuukagua uwanja huo mwishoni mwa mwaka jana.
    Viwanja vingine ambavyo vinatambulika na CAF pamoja FIFA kwa kutumika na michezo ya kimataifa ni pamoja “Amani wa Unguja, Zanzibar, Azam Complex na uwanja wa taifa wa Dar es Salaam”.
    Kupitishwa kwa CCM Kirumba kuna ongeza wigo wa kuwa na viwanja vingi vitakavyotumiwa na michezo ya mechi kubwa za kimataifa kama zile za fainali za Kombe la Shirikisho, Ngao ya Hisani pamoja na mechi kubwa za kimataifa za kirafiki na mashindano ya CECAFA, CAF na FIFA.

    Viwanja vingine ambavyo vimekaguliwa na na vinasubiri majibu ya kupitishwa kwake ni Gombani ulioko Pemba; Sokoine wa Mbeya na Kaitaba wa Kagera.

    No comments:

    Post a Comment